Mwanaume Aliyejitekeza Kwa Moto Kisa Ugumu wa Maisha Kenya Afariki Dunia

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Mwanamume aliyejulikana kwa jina Robert Gituhu aliyejiteketeza kwa moto Siku ya Jana (Alhamisi) akilalamikia ugumu wa maisha alifariki saa Nne na Dakika 20 Usiku wa Jana alipokuwa akipatiwa matibabu katika Hospitali Kuu ya Pwani, Coast General nchini Kenya.

Msimamizi Mkuu wa Coast General Iqbal Khandwalla amethibitisha kwamba mwanamume huyo aliyekuwa na umri wa miaka 27 alipata asilimia 80 ya majeraha ya moto na kwamba alifariki siku iyo hiyo aliyolazwa hospitalini.

“Madaktari wetu walifanya kila wawezalo, tulimpa dawa na matibabu mengine yaliyofaa, lakini kwa bahati mbaya alifariki saa nne na dakika 20 usiku,’ amesema Bw Khandwalla.

Kwenye video iliyosambazwa mtandaoni mwanamume huyo alionekana akiwa amebeba bendera ya Kenya kabla ya kujiwashia moto katika eneo la Mwembe Tayari, Kaunti ya Mombasa.

Marehemu alikuwa mhitimu wa Chuo Kikuu cha Nairobi. Alisomea taaluma ya uhandisi ambapo alihitimu mwaka 2021.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad