CCM yampa Waziri Mkuu miezi sita kumaliza migogoro ya ardhi

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

CCM yampa Waziri Mkuu miezi sita kumaliza migogoro ya ardhi


Chama cha Mapinduzi (CCM) kimemtaka Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kushughulikia kikamilifu kero za migogoro kwa kipindi kisichopungua miezi sita.


Kauli hiyo ya chama imetolewa leo Novemba Mosi, 2023 na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Paul Makonda alipokuwa kwenye mkutano wa hadhara jijini Dodoma.


"Chama kinamuelekeza waziri mkuu ndugu Kassim Majaliwa kusimamia kikamilifu suala la kutatua migogoro ya ardhi kwa kuunganisha wizara tatu chini ya wizara mama ya ardhi.


"Wizara ya TAMISEMI inayo migogoro inayotokana na mipaka, Wizara ya Mariasili inayo migogoro inayotokana na mipaka ya hifadhi na wizara yenyewe ya ardhi inayo migogoro ya ardhi.


"Chama kinamtaka Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ndani ya miezi sita awe amesimamia na kuratibu kikamili, kuondoa na kufuta migogoro yote ya ardhi inayopelekea wavuvi, wakulima, wafugaji na wananchi kuteseka ndani ya ardhi yao," alisema Makonda.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad