Polisi Yazima Tukio Kubwa la Ujambazi Kigamboni

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Polisi Yazima Tukio Kubwa la Ujambazi Kigamboni

 

Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, limefanikiwa kuzima tukio la ujambazi uliopangwa kufanyika katika eneo la Kampuni ya Kijiji Park, iliyoko Kibada Kigamboni, wilayani Temeke, Mkoa wa Dar es Salaam.


Akizungumza na waandishi wa habari jana tarehe 17 Novemba 2023, Kamanda wa kanda hiyo, ACP Jumanne Muliro, amedai kundi la watu sita wanaodaiwa kuwa majambazi wakiwa na silaha za jadi, walivamia eneo hilo usiku wa jana Alhamisi, kwa lengo la kutaka kuiba mafuta yaliyohifadhiwa chini ya ardhi.


Kamanda Muliro amedai kuwa, kundi hilo baada ya kuingia ndani ya eneo wakiwa na gari aina ya fuso walianza  kumfunga kamba mlinzi kisha kuanza kuiba mafuta. Lakini kabla hawajamaliza polisi walifika na kuanza kuwadhibiti.


“Jeshi la Polisi baadae lilipata taarifa toka kwa watu wema na kufika haraka eneo la tukio.Alikutwa mlinzi akiwa kwenye hali mbaya akaokolewa na baadae wahalifu hao walijaribu kuwashambulia askari ambao walijihami haraka na kuwajeruhi wawili miongoni mwao kwa risasi,” amesema Kamanda Muliro na kuongeza:


“Watuhumiwa hao walipelekwa hospitali wakiwa na hali mbaya na majina yao hayajafahamika. Mtuhumiwa mwingine  aliyekamatwa eneo la tukio ni Nelson Mbewe (49), mkazi wa Ubungo Kibangu na anahojiwa kwa kina juu ya tuhuma hizo za unyang’anyi wa kutumia silaha kwa kuvamia eneo hilo. Wahalifu wengine wanaendelea kusakwa na lazima watakamatwa.”

----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad