AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
SERIKALI imesema wanafunzi wote waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza katika Shule za Serikali kutwa na bweni hakuna atakayekosa nafasi kwani Serikali imetenga Sh bilioni 140.5 kwaajili ya ujenzi wa madarasa mapya sambamba na ukarabati wa madarasa yaliyopo kuelekea muhula mpya wa masomo utakaoanza Januari 08, 2024.
Hayo yametanabahishwa na Waziri Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mohamed Mchengerwa katika taarifa yake kwa umma katika mkutano wake na viongozi wa ngazi za Mikoa na Wilaya, uliofanyika ndani ya ukumbi wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza.
“Uchaguzi ulihusisha wanafunzi 1,092,984 wakiwemo wasichana 507,933 na wavulana 585, 051 ambao walifaulu mtihani wa kuhitimu Elimu ya Msingi mwaka 2023.” amesema waziri huyo.
Amesema vigezo vilivyotumika kuchagua wanafunzi hao ni kwa kuangalia waliopata alama za ufaulu kati ya 121 hadi 300, miongoni mwao hakuna asiyepangiwa shule.
“Idadi ya wanafunzi waliofaulu kujiunga na kidato cha kwanza Januari 2024 imeongezeka kwa wanafunzi 16,947 sawa na ongezeko la asilimia 1.57 ikilinganishwa na wanafunzi 1,076,037 waliopata alama za kuwawezesha kujiunga na kidato cha kwanza mwaka 2023.” Amesema Mchengerwa.
Amesema miongoni mwa waliofaulu na kupangiwa kujiunga na Kidato cha Kwanza Januari, 2024 wamo wanafunzi wenye mahitaji maalum 3,587 ambapo wasichana 1,590 na wavuala 1,997.
WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA KWANZA BONYEZA HAPA
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK