Shaffih Dauda "Simba Imeuzwa Mashabiki Mnalijua Hilo"

Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo Bonyeza Hapa


Ameandika haya Shaffih Dauda:

Tafsiri nyepesi baada ya kuisikia kauli ya Mfanyabiashara Mohammed Dewji .

1. Dewji sio Mwekezaji ndani ya Simba kama ambavyo siku zote ilikuwa ikifahamika bali ni Mmiliki wa Simba na anamiaka mitano sasa.

2. Simba SC ambayo mashabiki wanasubiri kukamilika kwa mchakato wa mabadiliko ili waishi kwenye 51% ya hisa wanapaswa kujua tayari timu hiyo imeuzwa na ni mali ya mtu na mwenye kuamua kubadilisha mfumo wa uendeshaji ni yeye bila shinikizo la mtu yoyote kwa sababu anaimiliki

3 Kwa kuwa ameinunua Simba SC ambayo ilikuwa timu ya wanachama maana yake Wanachama hawana chao ikiwapendeza wakubali kuwa chini ya tajiri iwe amenunua hadi hao wanachama [Mashabiki ] ambao nao sasa watakuwa mali ya Tajiri

Kama umepitwa na hiyo kauli hii hapa chini

“Nadhani kitu ghali zaidi nilichowahi kununua ni klabu ya mpira inaitwa Simba inamashabiki milioni 35, niliinunua hii klabu miaka mitano iliyopita, nimepoteza takribani Dola za marekani milioni 4 (Tsh bilioni 10.2) kwa mwaka mmoja na kwa miaka yote mitano nimepoteza Dola za marekani milioni 20 (Tsh bilioni 51).

NB: Nani amemuuzia Tajiri timu ?
_________

LOVE STORY YA UTANIKUMBUKA NEYLA Ipo tayari ni maandishi na Sauti !, Kuisoma yote Bonyeza HAPA Lipia tsh 1000 Tu mtandao wowote,au Tembelea www.makapedia.com

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad