AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Nyota wa Klabu ya Yanga, kiungo Stephanie Aziz Ki na kipa Djigui Diarra wametua kwenye kambi ya timu hiyo kuungana na wenzao kwa ajili ya maandalizi ya mchezo wa robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Mamelodi.
Awali akizungumza na wanahabari kuelekea mchezo huo, pamoja na majeraha waliopo kwenye kikosi chake, Kocha wa Yanga Miguel Gamondi alisema Aziz raia wa Burkina Faso na Diarra raia wa Mali hawajafika kambini licha ya kwamba aliamini wametua nchini alfajiri ya leo wakitokea kwenye majukumu ya timu zao za Taifa.
Aziz na Diarra wameshusha presha ya kocha Gamondi na mashabiki wa Yanga ambao walikua na wasiwasi itakuwaje kuwavaa Masandawana bila kuwa na wachezaji wao muhimu kwenye kikosi.
Yanga na Mamelodi watakipiga kesho Jumamosi katika Dimba la Mkapa majira ya saa 3 usiku.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK