FURSA ILIYOPOTEA:NINGEKUWA RAIS NINGEONGEA KISWAHILI ZIARA YA OBAMA

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Kiswahili hiki cha waswahili ni kama mwanaharamu huko pwani ya waswahili, masikini kimezaliwa wakati mama anajifungua akafa, kikalelewa na baba wa Kambo mwalimu Nyerere naye kwa kansa ya damu akafa.
Kiswahili aliachwa mdogo lakini mwenye afya njema akiendelea kukua, hongera kwa baba wa kambo ambaye kweli alimpenda kiswahili japo alimuua mke wake wakati akizaliwa. Kiswahili yatima ambaye sasa anabidi akue mtaani tena aitwe mtoto wa mitaani maana hata kanyaga tena ikulu wala hafla za kimataifa, labda Chissano alirejee kwenye madaraka huko nchi ya jirani Msumbiji. Hongera Chissano kukumbuka kiswahili japo TZ ulipita tu kuomba msaada wa kukomboa nchi yako, jasiri hakuacha kusahau mchango wa Kiswahili kufanikisha mambo ya Wamsumbiji.

Kwa nini tumeshindwa kutumia fursa nyingi ama zote kukistawisha kiswahili, lile baraza la kiswahili linakula tu fedha za watanzania au linafanya kazi gani??? halikumshauri hata rais kutumia fursa ya ujio wa obama kutangaza kiswahili?? au rais alikaidi?? rais si ni taasisi au huu utaasisi ni majibu ya kijanja janja kule kwa Makinda ANNE??? Hongera Kenyairways kututangazia Kiswahili duniani.

Kwa nini rais ataabike kiasi kile kuongea kiingereza wakati kiswahili kipo? hata kama rais angekuwa mzuri sana kwa kiingereza Je haikuwa fursa ya kutangaza utaifa wetu na kiswahili chetu?? hivi wajapan, wachina, warusi na waarabu wakiongea lugha zao ni kwambma hawajui kiingereza kabisa, au wanataka kuweka alama sahihi juu ya wao ni kina nani, kujitambulisha kwa dunia kuwa ni mataifa huru yenye lugha zao huru kwa matumizi yao. Kiswahili umekosa mvuto huo nyumbani na ugenini. pole haya yote yanamwisho, ama siku ukijifia au siku ukikumbukwa fedheha kilemba cha ukoko.

Kweli watanzania mmetutenda tena sana, fursa moja ikipotea mikononi na mdomoni mwa ikulu, hi hatari sana maana inaweza isije tena kwa miongo kadhaa, washauri wa rais, ikulu mnafanya nini??? mnashauri nini?? mbona imekuwa kama mnamkomesha rais? aliwakosea nini sasa mnamlipa ubaya wote huo?? si aliwaaamini mmsaidie kazi?? Kwani kiswahili kitaongewa na nani kama sio rais na ikulu ya dar??? mtoto kiswahilil kakosa nini hadi anakataliwa kwao???

Naomba serikali ifikirie tena pengine iweke mikakati kuwa rais na ikulu waongee kiswahili kwenye shughuli zote zikiwemo za kimataifa, ipo siku aibu itakuwa kubwa, narudia hii tunaona ni harufu tu, ipo siku tutaona mzoga wenyewe.

Kiswahili Kiswahili nakupenda lugha ya taifa langu.

Naomba kuwasilisha.


Source
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

2 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Kweli inasikitisha kwanini hatutumii kiswahili sehemu muhimu kama hizi. nilimchek first lady akisoma hotuba kwa ngeli ile pronuotiotions yake daah! kuongea kiswahili ktk mikutano sio kujidhalilisha ila itaonesha tunajali utamaduni wetu.

    ReplyDelete
  2. Kweli inasikitisha kwanini hatutumii kiswahili sehemu muhimu kama hizi. nilimchek first lady akisoma hotuba kwa ngeli ile pronuotiotions yake daah! kuongea kiswahili ktk mikutano sio kujidhalilisha ila itaonesha tunajali utamaduni wetu.

    ReplyDelete

Top Post Ad