AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Kukatika kwa Mkonga huo kumesababisha vituo vyetu vya kutoa huduma za mawasiliano vilivyopo Oysterbay na mbezi juu kushindwa kufanya kazi kutokana na vituo hivyo kutegemeana kumesababisha kushindwa kutoa huduma za mawasiliano.
Kutokana na hilo wateja hawakuwa na uwezo wa kupiga simu, kutumia intaneti na hata huduma za kifedha. Tunatambua usumbufu ambao umetokea kwa kukosa mawasiliano, kwa mara nyingine tena tunaomba radhi na tunashukuru kwa uvumilivu wao katika kipindi chote ambacho huduma zilikosekana.
Mafundi wetu wameweza kurekebisha uharibifu uliotokea barabara ya Mwai kibaki ambao uliotokana na shughuli za ujenzi wa barabara zinazoendelea. Uharibifu mwingine uliotokea katika Barabara ya Mlalakuwa ulichukua muda kurekebisha kutokana na nyaya zilizo katika mkonga wa mawasiliano kuungua kulikosababishwa na zoezi la uchomaji taka lililokuwa linaendelea katika sehemu ambayo mkongo umepita na kusababisha uharibifu huo.
Napenda kuwahakikishia wateja wetu kuwa, Tumejidhatiti katika kuendelea kutoa huduma bora na za kipekee wakati wote watakapokuwa wanautumia mtandao wa Vodacom, Tunawashukuru kwa namna ambavyo wameendelea kutuunga mkono na kutuvumilia pale matatizo yanapojitokeza.
Rene Meza
Mkurugenzi Mtendaji – Vodacom Tanzania
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK
U dont need yo tell us blah blah hapa.tulipe fidia kwa usumbufu tulioupata.maana wengine wamefiwa na ndugu zao simply kwa kushindwa kuwatumia fedha za matibabu through Mpesa na wengine wamegombana na familia zao kwa kushindwa kuwa hewani.useless Tanzanian service providers!!! Simple statement umemaliza!!!real????
ReplyDeletekawaida sana hakuna haja ya kulaumu
ReplyDeletehata hivyo ilikuwa poa sana maana waliokuwa na miadi ya kuvunja amri ya sita walikwama
ReplyDeleteila kweli
Delete