Mwakyembe Amshambulia LOWASSA Kuhusu Sakata la Richmond...........Mwigulu Nchemba naye Adai Lowassa Ni Mpiga Dili Tangu Kijana

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Mwakyembe Akihutibia Umati
Aliyekuwa mwenyekiti wakamati teule ya bunge ya kuchunguza kashfa ya mkataba tata wa Richmond iliyomuondoa madarakani aliyekuwa waziri mkuu Mh Edward Lowassa, Mh Harrsion Mwakyembe amewahakikishia watanzania kuwa walijiridhisha pasipo shaka kuhusika kwa Edward Lowassa katika sakata la Richmond na kwamba hawakumsingizia kama anavyojitetea hivi sasa.

Mwakyembe aliyasema hayo mbele ya maelfu waliojitokeza katika mkutano wa hadhara wa mgombea urais wa CCM, Dk John Magufuli katika viwanja vya Luandanzovwe jijini Mbeya, jana.

Akizungumzia madai ya kwa nini baadhi ya wahusika hawakupelekwa mahakamani kama kuna ushahidi, mhadhiri huyo wa sheria alisema kosa la jinai, halina ukomo na wakati wowote linaweza kufunguliwa mashitaka, huku akiapa kuwa anaweza kumfungulia mtu mashitaka hata kesho.

Alionya viongozi na makada wa Chadema na vyama vinavyowaunga mkono katika umoja wa Ukawa wanaozindua kampeni zao leo jijini Dar es Salaam, kwamba wasithubutu kujibu hoja zake.

Dk Mwakyembe alisema ikilazimika kusema ukweli, ataweka hadharani uchafu wote uliofanyika, ambao alisema bungeni kuwa asingeuanika na kuifanya Richmond hoja ya kila siku mpaka Watanzania waelewe kilichofanyika.

“Tunao ushahidi. Hawa walitakiwa kuwa jela badala ya kuimba nyimbo za ajabu,” alisema Dk Mwakyembe katika mkutano huo uliorushwa moja kwa moja nchi nzima na kuongeza kuwa Dk Magufuli akiingia madarakani, anakwenda kuanzisha Mahakama ya Ufisadi.

Alisema yeye na wenzake walipewa kazi ya Bunge kuchunguza ilikuwaje viongozi waandamizi wakaamua kuipa kampuni hewa zabuni ya mabilioni ya fedha, ambayo imesababisha mpaka leo kuna shida ya umeme nchini.

Dk Mwakyembe alikumbusha kuwa walikwenda mpaka Marekani kuchunguza uwepo wa kampuni hiyo iliyodaiwa kutoka katika nchi hiyo, na kukutana na kampuni ya kuchapisha kadi za harusi.

Kwa mujibu wa Dk Mwakyembe, baada ya kubaini ubadhirifu huo, aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa, alishinikizwa kujiuzulu na kumaliza suala hilo na hivyo hatua ya kiongozi huyo kutaka kwenda Ikulu, wazalendo hawawezi kuikubali.

“Hatutaruhusu watumie demokrasia kuingia Ikulu na hiyo ndiyo shida ya kuazima wagombea,” alisema Dk Mwakyembe akimaanisha kuwa chama cha Chadema, kimeazima mgombea bila kumfahamu.
 
 Dk Mwakyembe alisema suala hilo lilishafungwa bungeni, lakini anashangaa kusikia linarejeshwa kinyemela.

Mwigulu
Naye Naibu Waziri wa Fedha na Uchumi, Mwigulu Nchemba, alisema mgombea wa Ukawa, Lowassa, tangu akiwa kijana alikuwa ‘mpiga-dili’.

Kwa mujibu wa Mwigulu, Rais Kikwete alipoingia madarakani, alidhani kuwa Lowassa alikuwa ameonewa, akamteua kuwa Waziri Mkuu, lakini kabla ya kumaliza miaka miwili, akaendeleza tabia yake ya ‘kupigadili’.

Mwigulu alionya kuwa, Watanzania wakimpeleka ‘mpiga-dili’ Ikulu, shida yake na wenzake si changamoto za watu wa Mbeya wapate maji, huduma bora za afya na nyingine bora za umma, bali kurejesha fedha walizotumia wakati wa kutafuta urais.

“Mkimpeleka mpiga dili Ikulu, ‘wapiga-dili’ wenzake hawatalipa kodi, mtalipa nyie wanyonge ili wale ‘wapigadili’ warejeshe fedha zao,” alisema na kufafanua sababu za vyama vya Chadema, CUF, NCCRMageuzi na NLD kuungana pamoja katika Ukawa.
 
Kwa mujibu wa Mwigulu, kilichowaunganisha ni maslahi ya aina mbili; moja aliyetoa fedha kwa ajili ya kwenda Ikulu, ambaye anatafuta nafasi hiyo ili arejeshe madeni yake na wengine ni waliouza vyama ambao ‘wameshakunja’ chao.

“Nawaambia mwisho wa mbwembwe na maigizo, ni Oktoba 25 na baada ya hapo ni kazi tu,” alisema Mwigulu na kuhoji iweje Lowassa apande daladala leo, ambalo hakulipanda miaka 40 iliyopita?
 
 Mwigulu alisema Watanzania wana siku 60 za kujadili hatima ya taifa lao na katika hilo, hakuna namna zaidi ya kuelezana ukweli mtupu.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

11 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Watanzania wanapenda mabadiliko.Wote waliingia madarakani wakiwa masikini wameondoka matajiri.Doctor Mwakyembe amekuwa mnafiki mkubwa sana.kwanini aianike hayo anayoyaita maovu ya lowasa kama kweli.nini kimemzuia asifungue mashitaka? vipi wahusika wa EPA,Escrow na uozo mwingine mwingi,kwani nini wahusika wanaachiwa bila sababu?
    Ajue kuwe tunaingiza Fisadi ikulu ili aibadilishe inchi kuliko kutuambia watu safi baadaye wanakuwa mafisadi.

    ReplyDelete
  2. Mwigulu senge kubwa hili limekaa kama nape oops mnyiramba wewe na usenge wako u na nini
    Mwakyembe wewe mungu alikupa rasharasha
    Tena toka ccm huko huko sasa utakoma leo jioni

    ReplyDelete
  3. ccm hamna jipya.

    ReplyDelete
  4. tunajivunia taifa kupata rais Lowasa mwenye afya imara!
    Yericko Nyerere 15:38 Today
    Makada wa ccm hasa wale wenye uelewa duni wanaendelea kupiga porojo juu ya Afya ya Mh Edward Lowasa, ni haki yao kutoa maoni ili taifa lipate rais bosa na mwenye afya bora.
    Lakini kinachoshangaza nikuona watu hawa wanajipa jukumu la utabibu na kusimulia kile wakiitacho “ugonjwa” wa Lowasa,
    Ukiwauliza Lowasa anaumwa nini? Hakika watakupa kila mtu jibu lake na ukimrudia tena mmoja mmoja kumuuliza atakwambia jibu tofauti na la awali, mara oooho Lowasa ana kisukari, mara ana kiharusi, mara ana kisend off nk, ilimradi tu waonekane wamesema.
    Ukiwauliza tena vipi afya ya Magufuli? Majibu yao ni kama wapo ahera vile,
    Hizi ndio siasa za kiswahili na waswahili wenyewe ndio sisi. Watanzania wengi huenda hawafahamu hili,
    Dr John Pombe Magufuli ni mgonjwa wa Moyo tangu mwaka 2000, na mwaka 2014 alikwenda kufanyiwa upasuaji mkubwa nchini ujerumani mjini Born, hivi hapo alipo Magufuli anatumia moyo wa bandia, na ikitokea mjanja yoyote yule aka hark software ya hospitali ile pale borne basi Magufuli ata stuck na kufa,
    Kila mwaka anatakiwa aende kuuchaji ambapo mwaka huu atakwenda 26/12/2015.
    Hilo wanaccm kindakindaki hawalifahamu, lakini Jakaya,Othuman, Mkapa, Pia Lowasa, Mbowe, na Madaktari bingwa wa moyo pale MOI wanajua vema.
    Masuala ya afya yakihojiwa sana kishabiki watu wawe tayari kupokea ukweli uliojificha!
    Mimi sijui ugonjwa wa Lowasa wala yeye hajui ugonjwa wangu bali madaktari wetu ndio hujua. Lowasa ni mzima, hakuna hospitali nchini na dunia iliyotoa taarifa za ugonjwa wake na kuwa hastahili kuwa Rais wa Tanzania

    ReplyDelete
  5. Inasikitisha sana kusikia kutoka kwako Mwakyembe tuhuma zinazomhusu Mhe. Lowassa leo!! NA HAPA NAAMINI KUMBE ULICHOFANYIWA WAKATI ULE NUSURA UFE KILIKUSTAHILI. Acha UNAFIKI, mwizi akiingia kwako kukuibia na ukafanikiwa kumdhibiti hatua inafuata ni kumlea au kumchukulia hatua za kisheria? Na je, kama siyo kumharibia mtu siku ni kwanini ulikaa kimya siku zote eti leo ndiyo unawaambia watanzania bila hata chembe ya haya ubaya wa Lowassa? Kwa kuwa hayupo CCM? uliponywa ili UTUBU HUO UNAFIKI WAKO usifikiri Mungu ni wa mchezo. UWAJIBIKAJI NDICHO KITU WATANZANIA TUNAHITAJI NA SIYO KUCHAFUANA.

    ReplyDelete
  6. Asante mwakyembe always wezi wanakuwa na sura za upole mwaka huu Lwasa afungwe.

    ReplyDelete
  7. wote nyie niwapigadili, kuna mtu huko juu ambaye cyo mpigadili?, achene hizo WATANZANIA cyo WADANGANYIKA tena, hata msemaje watu wameshaaamua!!!

    ReplyDelete
  8. Kweli wadau Mimi nawashangaa sana hawa wanao jiita wasafi.pia Wa zima Wa afya ivi endru change hakuwa reach mound aliyekuwa waziri Wa nishatinna mafini ngeleja na kambi take hawakuhusika karamagi hakuhusika mbona hao uwataji wewe mwakyembe mbona uwataji majizi ya escrow yaliyo anikwa wazi na yakakiri kweli walichota mapesa hao uwaoni ama siku wakihama ccm ndio wataonekana acha siasa zakishenzi wewe mwakyembe wewe ni pumbu tu una lolote of couze tunalipa kupitia Kofi zetu kwani hizo za escro za rada makaa yamawe aliyo iba Ndugu yako pumbu mwenzuo mkapa unazani zenyewe hatuzilipi mbona tunazilipa mpaka mmepandisha makodi ya kutisha nakuzidi kutugandamiza nakama kweli lowasa aliiba sibado mnamiliki nchi mnasubiri nini kumkamata kabla raising wako kikwete hajaachia nchi mbona katiba inaruhusu mkamateni at a Leo pale jangwani si mwizi bhana mnambakisha Wa nin mtangulizeni mahakamani ukunyuma tukiwaletea hao mnao walinda wazee Wa vijisenti na vijimboga nyoko wewe mwakyembe uyo uyo mwizi ndio tunae mtaka atakama ni zimwi mla watu ni maiti tunaitaka na tutakaa mayo ikulu na tutaizika wenyewe

    ReplyDelete
  9. Heeee Lowasa kikwete wote wezi na mwakyembe asingeweza kuyasema hayo alikua anamuogopa kikwete,,,, Tusidanganyike lowasa damu ya ccm na hatoacha wizi ndio maana anahangaika yeye na sumaye waingie ikulu waibe vizuri kwa kujinafasi,,,,, UKAWA TUAMBIENI KIPI KILICHOMFANYA LOWASA AWE MSAFI? NA TUNAMTAKA DR SLAA AMSAFISHE KAMA ALIVYO MCHAFUA MIAKA YOTE,,,, PAMOJA NA KWAMBA MNATUKANA WATU WANA AKILI MGANDO HAIJALISHI,, ikilu ataingia kwa ku download habari ndiyo hiyo.

    ReplyDelete
  10. DUH KWELI WATU WAMECHOKA WANATUKANA HIVYO....na haka kasheria kenu ka makosa ya mitandao sijui kama kata DO kweli

    ReplyDelete
  11. Hana jipya huyo, ccm siasa za kupakana matope zitawagharimu

    ReplyDelete

Top Post Ad