Zari Awapiga ‘Stop’ Ndugu wa Mwanamuziki Diamond Platnumz

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Imelda Mtema
Stop! Wakati akisubiriwa kujifungua muda wowote, mwandani wa staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ anadaiwa kuwazuia baadhi ya ndugu wa jamaa huyo kuingia kwenye chumba maalum kilichoandaliwa ili kuepuka kisiingie vumbi na kiwe safi wakati wote.

Chanzo chetu ambacho ni mmoja wa ‘memba’ wa familia hiyo kilipenyeza kuwa, kwa sasa nyumbani kwa mwanamuziki huyo maeneo ya Madale-Tegeta, Dar, wana bashasha wakimsubiria mtoto huku chumba hicho kikiwekewa uangalizi mkubwa.
“Yaani Zari hataki mchezo kabisa na haruhusu mtu kuingia chumbani humo hovyo kwa sababu ya kuepuka vumbi kwa mtoto kwa maana chumba hicho hakihitaji msongamano wa watu wengi,” kilisema chanzo hicho.

Mpashaji huyo aliweka wazi kuwa, Zari alitia ngumu na kusema ni sheria aliyoiweka mwanamama huyo na haitakiwi kukiukwa na mtu yeyote kwa kuwa wanafahamu fika kuwa chumba cha mtoto hakihitaji msongamano wa watu hivyo ndugu hao imebidi wawe wapole.
Kilidai kwamba, kwa sasa kila mtu anayefika nyumbani hapo anahojiwa na kwamba kama siyo ndugu wa ndani zaidi kwenye familia haruhusiwi hata kuingia getini.Akizungumza na Ijumaa Wikienda kuhusu maandalizi hayo, Diamond alisema kila kitu kipo sawa na kwamba, anamuomba Mungu mambo yaende kama alivyopanga.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

19 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. stupid ngoja wazae kioja

    ReplyDelete
  2. MTAIONA JUNE JULYY
    HAPO NI ONLY FIRST BLOOD HAKUN AUDUGU WA KUPANGA.
    HAHAHA MLIZOWEA BINTI SEPETUNGA HANA NENO FAMILY IS FAMILY.
    HAPO MKO KWA MGANDA!!!

    ReplyDelete
  3. Domo atavumiliaaaaaaaaaaa, iko siku atachoka anafikiri kwa Wema family yoote inalala kwake, wasubiri azae ndo watamjua mganda kafata nini kwa Almas.

    ReplyDelete
    Replies
    1. Atavumilia nini na wewe? Zari anawaumaje roho sasa? Kwa taarifa yako wewe na mburulaz wenzako. Domo na Zari walikuwa wanawapotezeni step kwa kuwaambia mtoto angezaliwa june au july. Mkaingia kichwa kichwa. Kumbe muda walikuwa wanaujua wao wenyewe. Kama hataki zogo asiseme?? There is only 1 boss lady kwa Domo. And thats Zari. Katafute ndimu....

      Delete
  4. Shangazi kaanza kupata kiwewe siku za kuzaa zinayoyoma, kaona aanze kuwa stopisha ndugu kwanza, ili mahesabu yakae sawa.

    ReplyDelete
    Replies
    1. Na wewe wastopishe ndugu zake huyo muuza togwa wako. Uwe na shangazi kama Zari wewe? Shangazi zako design za Halima muuza shanga kama si Mwanaharusi mstutaji. Ndo maana umeishia kuwa mkewe huyo bwege anaekukoleza kwenye kitanda chenu kisichoeleweka. Mkome Zari.

      Delete
  5. ANAJUA KAMDANGANYA DAI, SASA NA NDUNGU WAKIANZA KUJILETA WATAJUA JANJA YAKE KAONA ISIWE TABU NGOJA ATUMIE MBINU MPYA.

    ReplyDelete
  6. walitangaza atazaa june, mara july naw august, sasa hakuna ndugu wa domo kuonekana eneo la tukio! yetu macho.

    ReplyDelete
  7. Nimeishi na waganda sio watu ni wachoyo balaa

    ReplyDelete
  8. Kwa raha zenu zari wabanie hao ndugu ndio wanao vunja ndoa za watu najua nyie bado mnazini hamjaoana ila wape ka Distance kido wa tie akili.

    ReplyDelete
  9. waganda ni kiboko. tusubiri tutaskia na kuona mengi. nahisi domo pia anaishi kwa masharti huko ndani kwake. na bado. domo aombe sana mkwanja usikate maana atanyang'anywa mtoto siku akichalala.

    ReplyDelete
    Replies
    1. Ukimaliza kuhisi kakojoe ukalale. Zari ana waweka macho eeh. Na bado mpaka mtanyooka..halalala

      Delete
  10. awape Distance kwani huyo zari anatumia pesa zake? kila kitu cha dai yeye anapanua tuu.

    ReplyDelete
    Replies
    1. Na wewe tafata wa kumpanulia. Ukibahatika sana utampata DJ wa vigodoro kama si mpishi wa pilau za hitima.mcxxx

      Delete
  11. NADHANI KWA KAWAIDA YA TAMADUNI ZA KITANZANIA, NDUGU NI BORA KULIKO KITU CHOCHOTE KILE. ILA KILA MTU ANA TARATIBU, KANUNI NA SHERIA ZAKE KATIKA KUISHI. WAFUATE MASHART YA MAMA MWENYE NYUMBA

    ReplyDelete
  12. hahaha diamondo unajitahidi kutujibu humu.
    kweeee

    ReplyDelete
  13. Dai anajitahidi kumjibu kila comment inayomsema bi kizee wake, kakaa kama Sinta anafikiri hatumjui bwana mipasho ya kwamtogole, umeruka mavi umekanyagaxxxx malizia basi kiki zinafiki pabaya kwamganda.

    ReplyDelete
  14. Dai anajiona ana akili saana, kaona ajaribu kujibu comment ili ionekane watu wanampenda zari, kaa ufirkiri mtoto ni wakatunzi au ivan, maana bi kizee kakitombesha kuliko wema.

    ReplyDelete

Top Post Ad