Milioni 50 za Rais Magufuli Kila Kijiji Zazuzua Kizaazaa

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


WAZIRI wa Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu, Jenista Mhagama alisema serikali imeweka utaratibu mzuri wa fedha za ahadi ya Rais ya milioni 50 kila kijiji, ili Watanzania wote wanufaike bila kujali itikadi zao za kisiasa.


Alisema hayo bungeni mjini Dodoma jana wakati akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Buyungu, Kasuku Bilango(Chadema) aliyetaka kusikia kauli ya serikali juu ya mgawanyo wa fedha hizo akisema ipo mizengwe kwamba fedha hizo zitatolewa kwa wanachama wa CCM .


“Serikali itoe kauli fedha hizo zitatolewa kwa utaratibu gani,” alihoji.


Mhagama alisema fedha hizo ni ahadi ya Rais aliyotoa wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu ambao Watanzania walichagua Serikali ya CCM.


Alisema serikali inatumikia Watanzania wote bila kujali itikadi za vyama vyao.


Alisema Baraza la Uwezeshaji Kiuchumi limeanza kutengeneza utaratibu wa namna ambavyo fedha hizo zitanufaisha Watanzania wote.


Alisisitiza kuwa serikali iko imara kuhakikisha fedha hizo zinanufaisha Watanzania wote.


Awali, Mbunge wa Viti Maalumu, Halima Bulembo (CCM), katika swali la msingi, alitaka kufahamu ni lini ahadi hiyo ya kutoa Sh milioni 50 kwa kila kijiji itatekelezwa.


Alitaka kufahamu pia vijana watapata mgao wao kwa asilimia ngapi.


Mbunge huyo pia alitaka kujua mikakati ya serikali katika kuwawezesha vijana wawe wajasiriamali kwa kuwapa mitaji, mikopo na vigezo gani vitakavyosimamia na kuwalinda na kuweka usawa wa upatikanaji wa ushiriki wao katika fursa hizo.


Akijibu swali hilo, Naibu Waziri wa Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu, Antony Mavunde alisema ahadi ya Rais ya Sh milioni 50 kwa kila kijiji itaanza kutekelezwa kwa mwaka wa fedha ujao 2016/2017.


Alisema utaratibu wa kugawa fedha hizo unaandaliwa na Baraza la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi kwa kushirikiana na Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

4 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. oops CCM
    thats our money all tanzania
    its nothing to do with ccm policy
    hizi ni pesa za watanzania wote na wala si za ilani ya ccm
    nashindwa kuwaelewa watanzania kuwachaguwa tena , japokuwa rais ni mzalendo pamoja na mizengwe na ya kuwa kuupata urais 2015 ilivyokuwa
    Magufuli hawezi kufanya kazi ndani ya CCM
    MMEMTOA KAFARA CCM ILI MPATE YENU
    HE IS THE BEST PRESIDENT IN TANZANIA AFTER MWL

    ReplyDelete
  2. oops CCM
    thats our money all tanzania
    its nothing to do with ccm policy
    hizi ni pesa za watanzania wote na wala si za ilani ya ccm
    nashindwa kuwaelewa watanzania kuwachaguwa tena , japokuwa rais ni mzalendo pamoja na mizengwe na ya kuwa kuupata urais 2015 ilivyokuwa
    Magufuli hawezi kufanya kazi ndani ya CCM
    MMEMTOA KAFARA CCM ILI MPATE YENU
    HE IS THE BEST PRESIDENT IN TANZANIA AFTER MWL

    ReplyDelete
  3. we need tanzania policy for our MONEY

    ReplyDelete
  4. its our money we need it
    shame you CCM
    mmezoea kudanganya watu fyuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuu
    eti ilani ya CMMMMMMM
    its CCCCCCCCCCCCCCCCCCCMMMMMMMMMMMMMMM
    money

    ReplyDelete

Top Post Ad