AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Ngoma ya ‘Natamba’ ilikuwa namba mbili trending siku ya jana YouTube, ila kutokana na hali ya sinto fahamu ngoma hiyo imepotea katika mtandao huo na kushuka kabisa katika nafasi iliyokuwepo.
Kwa mujibu wa meneja wake MX Carter ameripoti kusikitishwa na tukio hilo na amedai kuwa kuwepo kwa watu wasiopenda maendeleo ya msanii huyo na kuamua kuiripoti ‘Natamba’ ishuke Youtube.
“Naona wabaya wasiopenda maendeleo ya AslayIsiaka wamereport video ishuke YouTube… bahati nzuri team ya ufundi inajitaidi kuweka sawa,” ameandika Mx katika Twitter.
Akaongeza kuandika katika mtandao wa Instagram “Poleni kwa mnaopata usumbufu kuiona Video mpya ya AslayIsihaka kama ujumbe unavyoongea hapo juu tuko kwenye jitiada za kuirudisha popote ilipokuwa ikionekana haswa kwenye trending mungu akipenda. Video imekuwa reported na iko Undereview na Youtube na tunajitaidi kuiweka sawa! Ukitaka kuangalia video ya aslay for Now ingia kwenye Bio yake au Search on YouTube.”
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK