Watu 2,624 Waathirika na Mafuriko Dodoma

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Dodoma. Mbunge wa Chemba (CCM), Juma Nkamia amewaomba watu wa kada mbalimbali kutoa msaada kwa wananchi wa kata ya Mrijo mkoa wa Dodoma walioathirika na mafuriko yaliyotokana na mvua zinazoendelea kunyesha.

Akizungumza na waandishi wa habari bungeni leo Januari 17, 2018, Nkamia amesema jana wananchi wengine 161 wamekosa makazi kutokana na nyumba zao kuzingirwa maji.

Amesema watu hao 161 wamefanya idadi ya wasio na makazi katika kata hiyo na kuhifadhiwa  na ndugu na katika shule kufikia 2624.

Amesema vijiji vilivyoathirika ni Mrijo Chini, Kaloleni na Olborot, “Lakini hadi sasa hakuna watu wanaohusika na maafa waliofika kutoa msaada kwa wakazi hawa. Waliotoa msaada ni msalaba mwekundu tu tena wachache.”

“Msaada unaohitajika ni wa mahema, vyakula na mahitaji mengine ya binadamu.”

Mwananchi
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad