Mtoto wa Ray Apata Dili Nono NMB Ateuliwa Kuwa Ubalozi

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Mtoto wa Ray Apata Dili Nono NMB Ateuliwa Kuwa Ubalozi
MTOTO wa Staa wa Filamu Bongo, Vincent Kigosi ‘Ray’, aitwaye Jarden Kigosi, amepata shavu la Ubalozi wa Benki ya NMB, ambapo amemfungulia akaunti kwa ajili ya kuhakikisha wanamwekea fedha zitakazokuja kumsaidia baadaye kwenye masomo yake na maisha ya baadaye.

Akizungumza na Global Publishers wakati wa kumfungulia akaunti hiyo, Makao Makuu ya Benki ya NMB, Posta jijini Dar, Ray alisema kuwa, amefurahishwa na hatua ya benki hiyo kumtumia mwanaye kama mmoja wa mabalozi jambo ambalo hata yeye alikuwa akilitamani sana japo hakujua wapi angeweza kumfungulia akaunti kwa ajili ya maisha yake ya badaye.

“Niwaombe tu mastaa wenzangu kuwa, suala la mtoto kumfungulia akaunti benki ni ya muhimu sana kwani sisi wazazi tupo leo lakini hatujui kesho yetu itakuwaje?

“Ili usimnyime haki ya maisha mazuri mwanao hapo baadaye, basi ni jukumu la kila mmoja kuhakikisha anamfungulia akaunti mwanaye ila hata asipokuwepo ataweza kusoma bila shida,” alisema Ray.

Ray aliambatana na mzazi mwenzake ambaye pia ni msaniiwa Bongo Movies, Chuchu Hans katika utambulisho wa mtoto wao Jarden kama Balozi wa NMB.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad