Zaidi ya Shule Ishirini Zachomwa Moto Kwenye Mapigano DR Congo

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Zaidi ya Shule Ishirini Zachomwa Moto Kwenye Mapigano DR Congo
Takriban shule ishirini zimechomwa moto kutokana na mapigano yanayoendelea Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Kwa mujibu wa habari,ndani ya wiki mbili zilizopita shule za msingi na sekondari zimekuwa zikiangamizwa kwa moto katika mapigano ya kikabila kaskazini mashariki mwa DRC.

Afisa polisi Ivan Legu amekiambia kituo cha habari cha Anadolu kuwa zaidi ya shule 60 zimefungwa katika vijiji sita eneo la  Djugu,Ituri.

Hii ni kutokana na mapigano na mashambulizi ambayo yamekuwa yakifanywa kati ya jamii za Lendu na Hema.

Zaidi ya watu arobaini wamepoteza maisha katika mapigano hayo,hali iliyoilazimu serikali kutuma majeshi kutuliza ghasia lakini bado haikusaidia.

Eneo la Ituri linaongoz katika mapigano ya kikabila na kusababisha vifo vya wengi.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad