SABABU ZA UGOMVI BAINA YA MAPACHA WA P-SQUARE ZAFAHAMIKA, SOMA HAPA

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Taarifa juu ya ugomvi ulioibuka wiki iliyopita baina ya ndugu mapacha wa kundi la P-Square Peter na Paul na kaka zao zimewashtua mashabiki wao walioko pande mbalimbali za dunia. Chanzo kimoja cha karibu na ndugu hao kimeelezea sababu na kile kilichotokea.

Inadaiwa kuwa ugomvi wa wanandugu wa familia ya Okoye ulianzia kwa wasaidizi wao binafsi, ‘Personal Assistants’ (PA’s).
 Ripoti kutoka katika vyanzo mbalimbali vya Nigeria zinasema kuwa ‘PA’ wa kaka yao mkubwa Jude aitwaye Wande alimpatia ‘PA’ wa Peter aitwaye Shege, pesa ili akamsajilie gari lake, lakini inasemekana ‘PA’ wa Peter badala ya kutumia pesa hizo kwa kazi aliyoelekezwa alizitumia kwa kitu tofauti. 
 Baada ya hapo inadaiwa kuwa ‘PA’ wa Jude alikasirika baada ya kugundua kuwa pesa alizompa ‘PA’ wa Peter hazikufanyiwa kazi aliyoelekeza. Alipoenda nyumbani kwa Okoye’s ‘Squareville’ ili kukabiliana na ‘PA’ wa Peter ndipo ugomvi ulizuka baina ya wasaidizi hao wawili wa ndugu.
 Chanzo kinaendelea kusema baada ya ugomvi kuanza Peter aliingilia na kutaka kumpiga msaidizi wa Jude hadi Paul alipoingilia kwa lengo la kuwaachanisha, lakini badala yake Peter alijikuta akimpiga ngumi pacha wake Paul na kuanguka chini japo inadaiwa kuwa Paul hakumrudishia ngumi kaka yake, na badala yake kaka yao mwingine aitwaye Tony naye aliingilia na kuanza kupigana na Peter. Wakati haya yote yanatokea mke wa Paul Anita alikuwa akishuhudia.
 Chanzo kiliongeza kuwa Peter anataka awe mhusika mkuu wa maswala ya fedha za kundi au apate mgao mkubwa zaidi, huku upande wa pili inadaiwa Paul anataka kaka yao mkubwa ambaye pia ni meneja wao Jude aendelee kuwa msimamizi mkuu wa maswala ya fedha zao kama ilivyokuwa miaka yote iliyopita, lakini mpaka ilifikia hatua ya kutaka wagawane mali kila mtu awe na chake.
 Baada ya habari za ugomvi baina ya wana ndugu hawa kuenea, hii ni post ya Paul aliyoiandika juzi kupitia ukurasa wake wa Facebook. 
 “After the storm comes the calm. Hoping for better days ahead as one family. God’s intervention.”
BONGO 5
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. mkishaoa tu kila kitu kinaharibika huwa sielewi kwa nn mmejiunga miaka kibao leo kuoa tu kila mtu awe na chake lol, hata hivyo mi naona mngefanya kazi pamoja the end of the time mgawane faida ingekuwa poa

    ReplyDelete

Top Post Ad