SITTA AIFUATA UKAWA ZANZIBAR KUNUSURU BUNGE

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Wakati viongozi wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) wakiweka kambi Zanzibar, Mwenyekiti wa Bunge Maalumu la Katiba, Samuel Sitta jana naye alitumia siku nzima visiwani humo akikutana na baadhi ya viongozi wa Serikali, katika kile kinachotafsiriwa kuwa kulinusuru Bunge hilo.

Habari zilizolifikia gazeti hili kutoka Zanzibar zinasema Sitta alikutana na Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein, Makamu wa Kwanza wa Rais, Maalim Seif Sharif Hamad, Rais Mstaafu, Aman Karume na mwanasiasa wa siku nyingi wa CCM, Mzee Hassan Nassor Moyo.

Zanzibar kwa sasa ndiyo moyo wa upatikanaji wa Katiba Mpya kutokana na wajumbe wake katika Bunge kutegemewa ama kuipitisha au kuikwamisha kwa kuwa kila upande kati ya mbili zinazovutana, hauna uhakika wa kupata theluthi mbili za kura.

Baada ya kuondoka bungeni na kutangaza kususia vikao vya Bunge hilo Aprili 16, mwaka huu, siku mbili baadaye viongozi wa Ukawa waliingia Zanzibar wakitaka kufanya mikutano ya hadhara kuwaeleza wananchi sababu za kufanya hivyo, lakini wakazuiwa na polisi na hadi jana walikuwa wanasubiri kibali.

Safari ya Sitta

Katibu wa Bunge Maalumu, Yahya Khamis Hamad pamoja na kuthibitisha ziara ya Sitta Zanzibar kuwa alikuwa akutane na Dk Shein, alisema hafahamu lolote kuhusu mkutano wake na Maalim Seif ambaye pia ni Katibu Mkuu wa CUF.

“Sifahamu malengo ya safari wala walichokwenda kuzungumza, ila ni kweli kwamba alifika Zanzibar leo (jana) na alitarajiwa kuondoka jioni kurejea Dodoma,” alisema Hamad na kuongeza:

“Hilo la kuonana na Maalim Seif silifahamu ila ninachojua aliniambia nimfanyie miadi ya kuonana na Dk Shein na nikaifanya kama alivyoelekeza.”

Mapema habari zilizolifikia gazeti hili kutoka Zanzibar zilisema, Sitta baada ya kukutana na Karume, Shein na Mzee Moyo alitarajiwa kukutana na Maalim Seif saa 9:00 alasiri.

Katibu wa Maalim Seif, Issa Kheri Hussein alithibitisha kwamba Sitta alikutana na kiongozi huyo nyumbani kwake, Mbweni saa 9:30 alasiri jana, lakini alidai kutokuwa na taarifa za mazungumzo hayo.

“Hilo naweza kulithibitisha kwamba mkutano huo umefanyika lakini mazungumzo yenyewe yalikuwa ya faragha na mimi baada ya Sitta kufika niliondoka, hivyo sikuweza kufahamu kilichozungumzwa kwa undani, pengine mpaka nizungumze na Maalim mwenyewe,” alisema Hussein.

Ziara ya Sitta kwenda Zanzibar imekuja wakati ambao kumekuwa na wasiwasi mkubwa wa kukwama kwa vikao vya Bunge hilo kutokana na msimamo wa Ukawa.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

2 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. wwajinga tu unasusia bunge mnajisusia wenyewe?

    ReplyDelete
  2. nyie waongo na msirudie kutoa post zaungo jna alikuwa bungeni hadi saaa mbili na nusu

    ReplyDelete

Top Post Ad