Mtuhumiwa Auawa kwa Kuchomwa Moto Baada ya Kushindwa Kujieleza

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

MTU mmoja mwenye umri kati ya miaka 25 na 30 ambaye jina lake halifahamiki, ameuawa baada ya kushindwa kujieleza juu ya pikipiki ambayo yeye na mwenzake walikuwa wanajaribu kuiuza Chalinze.

Watu hao walifika Chalinze wakidai kutokea Gairo wakitaka kuuza pikipiki aina ya Toyo yenye namba za usajili T 336 BZC.

Lakini walipobanwa kuhusu kadi ya pikipiki walibabaika na hivyo kuanza kupigwa ambapo mmoja alitoroka na huyo mwingine kuuawa kwa kuchomwa moto baada ya kipigo.

Tukio hilo limethibitishwa na kaimu kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Athuman Mwambalaswa.

Kamanda huyo alisema kwamba tukio hilo lilitokea Septemba 25 mwaka huu, majira ya saa 1 asubuhi eneo la Pera Chalinze wilaya ya Bagamoyo.

Kamanda huyo aliwataka wananchi kuacha kujichukulia sheria mkononi kwani ni kinyume cha sheria na kuwataka kuwapeleka kwenye vyombo vya sheria, ikiwa ni pamoja na polisi ili hatua stahiki ziweze kuchukuliwa.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. kama pikipiki ilikuwa yao walikosa vip kadi???

    ReplyDelete

Top Post Ad