AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Kesi hiyo imefunguliwa katika Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dodoma ambapo mlalamikaji ni Godfrey Sabato John Wasonga dhidi ya TLS na Mwanasheria Mkuu wa Serikali.
Wasonga anaitaka mahakama ihairishe uchaguzi wa TLS hadi hapo Bunge litakapokutana mapema mwezi ujao kuweza kubadili kanuni zinazoongoza chama hicho.
Kwa taarifa za wadau kutoka kwenye mitandao ya kijamii zinadai kuwa hii ni njama ya Waziri Mwakyembe kumkwamisha Tundu Lissu kugombea urais wa TLS.
Waziri Mwakyembe hivi karibuni amenukuliwa akisema kuwa tatizo kubwa ni mtu mwenye kofia ya uongozi kwenye chama cha kisiasa kugombea urais wa TLS. Miongoni mwa wagombea ni Tundu Lissu ambaye pia ni Mwanasheria Mkuu wa CHADEMA ambapo tayari ana kofia ya uongozi kwenye chama cha siasa.
Aidha, inadaiwa kuwa, mabadiliko yanayotarajiwa kufanywa na Bunge kuhusu TLS ni kuzuia kiongozi wa chama cha siasa kuwania urais wa TLS.
Source: Swahilitimes
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK