KENYA: Uhuru Kenyatta Amesema Atakabithi Madaraka Kwa Wapinzani Ikiwa......!!!

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta, amesema ikiwa atashindwa kwa haki, Uchaguzi Mkuu wa tarehe nane mwezi Agosti, atakubali matokeo na kukabidhi madaraka kwa amani.


Rais Kenyatta ametoa hakikisho hilo wakati akijibu maswali mbalimbali kupitia runinga na kumtaka mpinzani wake Raila Odinga, naye kuwa tayari kufanya hivyo ikiwa atashindwa katika Uchaguzi huo.
Kenyatta amesisitiza kwamba, yeye ni mtu anayeheshimu uamuzi wa wananchi, na kuwaomba wapinzani wake nao wafanye hivyo.

Aidha, amesema serikali yake imelenga Uchaguzi huo uwe wa amani ndiyo maana maafisa wa usalama wamejihami na wako tayari kukabiliana na wale watakaotaka kuzua fujo.
Naye Bw. Odinga, anayepeperusha bendera ya muungano wa upinzani NASA, amekuwa akisema kuwa atakubali matokeo hayo ikiwa Uchaguzi huo utakuwa huru na haki.

Hata hivyo, hivi karibuni ametoa madai mazito kuwa Rais Kenyatta anatumia jeshi kumsaidia kuiba kura, madai ambayo serikali imekanusha.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad