Nyumba za Askari Zateketea Kwa Moto Mkoani Arusha

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Nyumba za Askari Zateketea Kwa Moto Mkoani Arusha
FAMILIA 13 zenye watu 44 zimeathiriwa kwa moto ulioibuka kwenye nyumba wanazoishi askari polisi katika Kata ya Sekei mkoani Arusha usiku wa kuamkia leo.
Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo ambaye pia aliwahi kufika eneo la tukio usiku huo amesema taarifa za awali zinasema chanzo cha moto huo ni hitilafu ya umeme na uchunguzi unaendelea. Gambo amesema hakuna mtu aliyejeruhiwa katika tukio hilo.

Mkuu wa Kikosi cha Zimamoto na Uokoaji mkoani Arusha, Andrew Komba amesema moto huo umeshadhibitiwa. “Tungefika mapema nusu ya nyumba zilizoteketea tungeziokoa,” amesema Komba.

Amesema taarifa kuhusu tukio hilo zimewafikia kwa kuchelewa. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Charles Mkumbo amesema hali ni shwari na hakuna wizi uliotokea. Amesema tukio hilo ni janga, hivyo watakaa kuona ni kwa namna gani watawasaidia  walioathiriwa.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad