Yanga Kuvana na Mtibwa Sugari Leo Yaahidi Ubingwa

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Yanga Kuvana na Mtibwa Sugari Leo Yaahidi Ubingwa
YANGA leo inacheza na Mtibwa Sugar katika Ligi Kuu Bara kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam, lakini imetamba kushinda.

Wakati Mtibwa ikiwa kileleni, Yanga yenyewe ipo nafasi ya sita ikiwa na pointi nane, lakini kocha msaidizi wa timu hiyo, Shadrack Nsajigwa amesema kuwa wamejiandaa kushinda mchezo huo.
Nsajigwa alisema wanataka kushinda mchezo huo ili kujiweka katika mazingira mazuri ya kutetea ubingwa wao.

Akizungumza na Championi Jumamosi, Nsajigwa alisema wanajua Mtibwa ni timu nzuri iliyojiandaa kwa ushindani msimu huu lakini watakabiliana nayo ili kuhakikisha wanapata ushindi.

“Tumejiandaa vizuri kwa ajili ya kuhakikisha tunapata matokeo mazuri katika mechi yetu na Mtibwa japokuwa naamini itakuwa na ushindani mkubwa kwani wapinzani wetu wapo vizuri msimu huu.
“Katika mechi hiyo tutamkosa Tshishimbi (Papy Kabamba ana kadi tatu za njano) lakini nafasi yake kuna mchezaji ambaye tayari tumemwandaa kwa ajili ya kuiziba hivyo ni matumaini yetu kuwa tutafanya vizuri,” alisema Nsajigwa.

Kwa upande wake, Kocha wa Mtibwa, Zuberi Katwila amesema moto walioanza nao msimu huu ndiyo huohuo watakaoendelea nao leo dhidi ya Yanga.
“Tunaiheshimu Yanga lakini kwa sasa sisi ni bora kuliko wao na ndiyo maana tunaongoza ligi kwa hiyo tumejipanga kuhakikisha tunaibuka na ushindi,” alisema Katwila.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad