Raia wa Korea Kaskazini Aiomba China Kutorudisha Nyumbani Familia Yake

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Raia wa Korea Kaskazini Aiomba China Kutorudisha Nyumbani Familia Yake
Raia mmoja wa Korea Kaskazini amemuomba rais wa China Xi Jinping kutomrudisha nyumbani mkewe na mwanawe wa kiume akisema kuwa watakabiliwa na kifungo jela au kifo iwapo watarudishwa Korea Kaskazini.
Mwanamke na mvulana wa miaka minne wanaeleweka kuwa miongoni mwa kundi la watu 10 wa Korea Kaskazini waliozuiliwa nchini China wiki iliopita baada ya kuvuka na kuingia nchini humo kisiri.
Mtu huyo ambaye alitaka kutambulika kwa jina la Lee pekee , alitorokea Korea Kusini 2015.
Alirekodi ombi lake katika mkanda wa video ambao uliwasilishwa kwa BBC.
Alisema kuwa mkewe na mwanawe watakabiliwa na hatia ya kifo ama kufungwa jela iwapo watarudishwa nyumbani Korea Kaskazini.
''Ningependa rais Xi Jinping na rais Donald Trump kumfikiria mwanangu kama kilembwekeza wao na kumleta mwanangu katika taifa huru la Korea Kusini '', alisema.tafadhali tusaidie.
''Okoa familia yangu kutorudishwa Korea Kaskazini. Mimi kama baba nawaomba viongozi hawa wawili kuisaidia familia yangu. Tafadhalini tusaidieni.Anasema kuwa anafuatwa na kiwiliwili cha mwanaye katika jela''.
''Nasikia sauti ya mwanangu ikiniita'', alisema.
''Namuona mwanangu katika jela ile baridi akimlilia babake, alisema.
''siwezi kusimama na kutochukua hatua yoyote''.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad