Utafiti: Je Unajua Jeraha la Mchana Hupona Haraka Kuliko Lile la Usiku

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Utafiti: Je Unajua Jeraha la Mchana Hupona Haraka Kuliko Lile la Usiku
Wanasayansi nchini Uingereza wamegundua kwamba majeraha ya kukatwa na kuchomeka hupona haraka yanapopatikana mchana ikilinganishwa usiku.
Wanasema kwamba ni kutokana na mwili unavyohisi kulingana na muda.
Utafiti huo unasema kuwa seli za ngozi ya mwanadamu hubadilisha tabia yake kulingana na muda huku protini zinazohitajika kurekebisha majeraha hayo zikifanya kazi vizuri wakati wa mchana.
Jeraha la kuchomeka nyakati za usiku lilichukua siku 28 kupona ikilinganishwa na siku 17 za jereha la wakati wa mchana.
Watafiti walitaja tofauti hiyo kuwa kubwa huku wakiongezea kwamba wanaweza kuharakisha watu kupona kwa kutumia dawa za steroids ambazo hubadilisha muda wa mwili.

Utafiti uliochapishwa katika jarida la Sayansi uliwahoji wagonjwa 118 katika kitengo cha wagonjwa waliochomeka nchini Uingereza.
Ulionyesha muda wa kupona wa 11 kati ya watu nyakati za mchgana na usiku.
Matokeo ya mahabara yalionyesha kuwa seli za ngozi kwa jina Fibroblast zilikuwa zikibadili uwezo wake katika kipindi cha saa 24

Seli hizo ndizo za kwanza zinazokimbia katika jeraha hilo ili kufunga kidonda.
Nyakati za mchana huwa zinafanya kazi sana na hupoteza nguvu hiyo nyakati za usiku.
Daktari O'neil mmoja ya watafiti aliambia BBC ''ni kama kukimbia mita 100''. Mkimbiaji hujiandaa kutoka , kawaida atamshinda yule aliyesimama akijiandaa kukimbia''.

----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad