Ewura Yatangaza Kupanda Bei ya Mafuta ya Taa, Petroli na Diezeli

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Ewura Yatangaza Kupanda Bei ya Mafuta ya Taa, Petroli na Diezeli
Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (Ewura), imetangaza kupanda bei ya mafuta ya taa, petroli na dizeli kulinganisha na Novemba Mosi, 2017.

Bei za rejareja za petroli, dizeli na mafuta ya taa zimeongezeka kwa Sh41 kwa lita sawa na asilimia 1.96; Sh30 (asilimia 1.54) na Sh3 (asilimia 0.17) kwa mfuatano huo.

Bei ya jumla ya petroli, dizeli na mafuta ya taa imeongezeka kwa Sh41.42 sawa na asilimia 2.06, Sh30 (asilimia 1.63) na Sh3.27 (asilimia 0.18) kwa mfuatano huo.

Kwa mujibu wa tangazo lililotolewa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Ewura, Godwin Samwel, ongezeko la bei kuanzia leo Jumatano Desemba 6,2017 limetokana na ongezeko la gharama za usafirishaji.

Amesema licha ya kuimarika kwa shilingi ya Tanzania dhidi ya dola ya Marekani fedha inayotumika kununulia mafuta, kumekuwa na ongezeko la bei ya bidhaa hiyo.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad