Jeshi la Polisi Lamkamata Mtuhumiwa Aliyeua Mkewe na Kichanga kwa Jembe

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Jeshi la Polisi Lamkamata Mtuhumiwa Aliyeua Mkewe na Kichanga kwa Jembe
JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limemtia mbaroni Ami Lukule, anayedaiwa kuwaua mke na mtoto wake kichanga cha umri wa miezi minane na mdogo wake wa kike, katika eneo la Matosa Darajani, Goba wilaya ya Kinodnini jijini Dar es Salaam wiki chache zilizopita.

Akizungumza na wanahabari leo Januari 16, 2017 jijini Dar es Salaam, Kamanda wa Polisi Kanda Maalumya Dar, Lazaro Mambosasa amemsema mtuhumiwa huyo alikamatwa hivi karibuni mkoani Iringa.

“Mtuhumiwa huyo tayari tumeshamkamata na baada ya kumhoji alikiri kufanya tukio hilo na kusema chanzo alikuwa mtoto. Amedai mkewe huyo alimtilia mashaka kwa kuingia kwenye mahusiano na mwanammme mwingine, anadai mke huyo alimzalia mtoto nje ya ndoa, hivyo akaamua kumnyonga mtoto na kufanya mauaji mengine mliyoyasikia,” alisema Mambosasa.

Aidha, Kamanda Mambosasa amesema kwa sasa wanafanya taratibu za kumsafirisha mtuhumiwa huyo kutoka Iringa hadi Dar ili kufikishwa mahakamani.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. sasa si angemuacha tu ona sasa ameharibu maisha yake ...

    ReplyDelete

Top Post Ad