Hili Hapa Tamko la IGP Sirro kwa Jamii

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Hili Hapa Tamko la IGP Sirro kwa Jamii
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro, ameitaka jamii pamoja viongozi wa dini kushirikiana na Polisi ili kutokomeza makosa mbalimbali katika jamii ikiwemo, mauaji yatokanayo na wivu wa mapenzi, ulevi, ubakaji ili kuiweka nchi salama zaidi.

IGP Sirro ameeleza hayo leo Jijini Dar es Salaam ambapo amesema kuwa takwimu za sasa zinaonyesha matukio ya aina hiyo yamekithiri sana nchini Tanzania jambo ambalo jamii inapaswa kubadilika ili kupunguza matukio hayo.

"Kuna makosa ambayo watu lazima wabadilike na hili haliitaji Jeshi la Polisi maana mimi nasimamia  Sheria lakini kuna viongozi wa dini wazungumzie hayo mambo. Muumini wako akija Kanisani au Msikiti na ukimwambia katazo la Mungu anaweza akabadilika", alisema IGP Sirro.

Kwa upande mwingine, Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Sirro amesema kuna makosa ambayo viongozi wa dini wakishiriki kwa ukaribu zaidi inaweza kupunguza huku akiitaka jamii kubadilika kitabia ikiwemo kuachana na ulevi wa kupindukia.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad