Kamanda Mambosasa Ajibu Kuhusu Watu Hatari kwa Taifa

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Kamanda Mambosasa Ajibu Kuhusu Watu Hatari kwa Taifa
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam Lazaro Mambosasa amefunguka na kujibu juu ya tuhuma alizotoa Mkurugenzi wa Kampuni ya CZI, Cyprian Majura Musiba kuhusu watu 10 aliodai ni hatari kwa usalama wa taifa.


Kamanda Mambosasa akiongea na waandishi wa habari leo Februari 26, 2018 amewataka Watanzania kutoshabikia habari kwenye mitandao ya kijamii na kudai kuwa habari zingine zinaandikwa na watu wenye upungufu wa akili lakini amedai kuwa wao taarifa hizo wamezipokea na kuzifanyia kazi kwani jeshi la polisi huwa linafanyia kazi kila aina ya taarifa kutoka kwa kila mtu.

"Niseme tu hao wanaodaiwa ni tishio kwa usalama wa taifa hizo ni taarifa sisi tukipokea huwa kwa kawaida hatupuuzii taarifa yoyote hata ingetolewa na kichaa, wapo vichaa wengi wanaendelea kuongea na kuposti mambo tunaendelea kuyapokea na kuyashugulikia mpaka tutakapogundua hili limeandikwa na kichaa tunaachana nalo, lakini niendelee kuwaomba Watanzania muendelee kulipa ushirikiano jeshi la polisi kwani tupo imara" alisema Mambosasa

Mbali na hilo Kamanda Mambosasa aliwashauri watu ambao wanakuwa na taarifa yoyote wahakikishe wanawafikishie wao jeshi la polisi ili waweze kuzifanyia uchunguzi zaidi

"Niwaombe pale ambapo wanasikia kwamba kuna tishio lolote lile waendelee kutoa taarifa kwa vyombo vya usalama tupo sisi polisi na wapo wenzetu wa usalama wa taifa lakini pia wapo viongozi mbalimbali katika ngazi tofauti hata serikali za mtaa wakiona ni vigumu kunifikia waendelee kutoa taarifa kwa watu hao kwani lengo taarifa hizo zifike sehemu ambayo taarifa hizo haziwezi kupotoshwa "


Mkurugenzi wa Kampuni ya CZI, Cyprian Majura Musiba jana alitaja orodha ya watu 10 ambao kwa mtazamo wake anasema kuwa ni watu hatari kwa usalama wa taifa na kusema kuwa watu hao wanapaswa kudhibitiwa, watu hao ni pamoja na Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, Mange Kimambi, Tundu Lissu, Zitto Kabwe, Julius Mtatiro, John Heche, Maria Sarungi, John Marwa, Evalist Chahari.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Kweli kabisa kutoka Na viashiria Na Historia Yao huko nyuma gani Hatari Na namuomgeza godiless pia...ila msigwa Ni data upepo Kama nassari. Huyu mvuya sigara bila chaps pia Ni mmojawapo

    ReplyDelete

Top Post Ad