AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Etienne Tshisekedi alifariki February 1, 2017 katika mji mkuu wa Ubelgiji, Brussels. Kutokana na kukosekana kwa makubaliano kati ya chama cha UDPS na serikali mjini Kinshasa, mwili wa Tshisekedi bado upo katika chumba cha kuhifadhi maiti mjini Brussels.
Kwa upande wa kambi ya Tshisekedi mjini Brussels, kipaumbele cha kwanza ni kurejeshwa kwa mwili wa Waziri Mkuu wa zamani nchini DRC, ambako anapaswa kuzikwa, katika moja ya sehemu ya familia yake katika eneo la N’Sele, mjini Kinshasa. Familia tayari imelipa Euro 16,000 kwa ajili ya kuendelea kuhifadhiwa kwa mwili wa Tshisekedi katika chumba cha kuhifadhi maiti cha Brussels.
Mitch Katumba, kiongozi wa chama cha UDPS mjini Brussels, amekua akikutana na viongozi wa Ubelgiji, Ufaransa pamoja na Ulaya, ili kuwezesha kurejeshwa kwa mwili wake nchini DRC. Mpaka sasa jambo hilo halijawezekana.
“Kabila, haipaswi kuwa na hofu, sio mwili wa Tshisekedi ambao utamuondoa madarakani, hakuna hoja yoyote kwa Tshisekedi kuzikwa nje ya nchi, Tshisekedi atazikwa DRC, katika mji wa Kinshasa. Tutajitahidi kusafirisha mwili wake,” -Katumba
“Sisi ni Waafrika, na sisi ni watu kutoka jamii ya Bantu. Kuna desturi, tuna maadili yetu. Mjane hawezi kukaa hivyo kwa mwaka mzima, wakati ambapo hatujamzika mumewe … Yuko hapo, analala chini, anaumia, ni mgonjwa, “ -Katumba.
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK