Amuuwa Mama Mkwe na Kumjeruhi Mkewe Kisa Unyumba

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Amuuwa Mama Mkwe na Kumjeruhi Mkewe Kisa Unyumba
Kijana aliyefahamika kwa majina ya Joseph Medardi (32) mkazi wa Nyakahanga Wilaya ya Ngara mkoani Kagera amemuuwa mama mkwe wake Elizabeth Simon (70) kwa kumkata kata mapanga na kumjeruhi mkewe Elice Joseph (28) kisha na yeye kujimwagia petroleum.


Kijana huyo amefanya tukio hilo kwa kile kilichoelezwa kuwa alikuwa na matatizo na mkewe kuhusu suala la unyumba jambo ambalo lilimpelekea kumrudisha mkewe huyo nyumbani kwa mama yake, ambapo amekaa huko takribani wiki tatu, siku moja kabla ya kikao cha kuwasuluhisha wanandoa hao ndipo kijana huyo ametekeleza mauaji hayo.

Mtoto wa marehemu Elizabeth Simon (70) ambaye ni Mchungaji Ezekia Simon amesimulia jambo hilo kwa undani zaidi na kusema kuwa chanzo cha yote hayo kuwa ni matatizo ya unyumba na kudai kuwa kijana huyo ambaye yeye ni shemeji yake alionekana amekuja na kusudio la kuwauwa wote yaani mama yake pamoja na mdogo wake huyo ambaye amejeruhiwa tu.

"Kisa cha kifo cha mama kimetokana na Mume wa dada kutoelewana katika habari za unyumba walikuwa na mgogoro kwa maana hiyo ikapelekea kumfukuza mkewe hivyo alikuja hapa yapata kama takribani wiki tatu yuko hapa nyumbani na baada ya hapo mimi kama Mkuu wa familia nilijaribu kutafuta njia ya kuwasuluhisha hivyo tarehe ambayo tulipanga kukutana ilikuwa jana ingawa hatukufanikiwa kukutana baada ya mzazi wa kijana kusema hakupata taarifa, matokeo yake yule kijana ndiyo amekuja akawashambulia mama pamoja na dada na kusababisha mauti ya mama"

"Yule kijana alikuja kwa lengo la kuuwa wale na yeye kujiuwa kwa sababu alipowashambulia na kuwajeruhi yeye alijimwagia Petroleum na kujichoma moto ndani ya nyumba hii hii"
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad