Madiwani Dar Walia na Itikadi za Kisiasa Kuwakwamisha Katika Maendeleo

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Madiwani Dar Walia na Itikadi za Kisiasa Kuwakwamisha Katika Maendeleo
Vitendo vya kuingiza itikadi za kisiasa vinavyofanywa na baadhi ya madiwani wa vyama mbalimbali jijini Dar es Salaam, vinadaiwa kukwamisha juhudi za maendeleo na huduma za kijamii kwa wananchi.

Wakijadiliana katika semina iliyoandaliwa na Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP), baadhi ya madiwani wa mkoa huo walisema itikadi hizo zimegeuka kuwa mwiba wa maendeleo.

Diwani wa viti maalumu kutoka Ubungo, Rehema Mayunga alisema linapokuja suala la kuwaletea maendeleo wananchi kila mmoja anapaswa kushirikiana na mwenzake.

Diwani wa Kivule, Wilson Molel alisema suala la kuingiza siasa katika kila jambo la maendeleo linachelewesha na kukwamisha miradi mingi, lakini waathirika ni wananchi.

Ofisa programu na uchechemuzi wa TGNP, Deogratius Temba aliwaomba madiwani kuhakikisha mikutano ya kisheria inafanyika kwa wakati na kuweka kwenye mbao za matangazo maazimio ya Serikali za vijiji na mitaa, mapato na matumizi ya fedha za umma.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad