Serikali ya Burund Yaipiga Marufuku BBC, VoA Kurusha Matangazo Nchini Humo

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Serikali ya Burund Yaipiga Marufuku BBC, VoA Kurusha Matangazo Nchini Humo
Serikali nchini Burundi kupitia Baraza la taifa la Mawasiliano (Conseil National de la Communation- CNC) imeyapiga marufuku mashirika mawili ya kimataifa ya utangazaji ya BBC na VoA .

Taarifa ya kufungiwa kwa mashirika hayo imetolewa leo Mei 04, 2018 na Rais wa Mamlaka ya Mawasiliano nchini humo, Karenga Ramadhan ambapo imesema kuwa mashirika mwisho wa kurusha matangazo yao nchini Burundi ni Mei 07 mwaka huu.

Sababu za mashirika hayo kufungiwa ni kufanya mahojiano na watu walioiasi Burundi wanaoishi ughaibuni na kuyarusha nchini humo kitu ambacho ni kinyume na sheria za mawasiliano na ni uchochezi.

Sambamba na adhabu hiyo, vituo vingine vitatu vya redio RFI, Isanganiro na CCIB FM vimepigwa onyo kali huku gazeti Le Renouveau la nchini humo likifungiwa miezi mitatu.

Sababu za kufungiwa kwa gazeti hilo ni kuandika habari ya kuandika makala zenye uchochezi zilizolenga kuikosoa serikali ya Rais Pierre Nkurunziza.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Top Post Ad