Wasichana Msiolewe na Wanaume Wanaoishi Mabondeni

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda, amewasihi wasichana katika mkoa wa Dar es salaam kutokubali kuolewa na wanaume ambao wanaishi katika maeneo ya bondeni ambayo ni hatarishi hasa katika kipindi cha mvua za masika.


Makonda amesema hayo leo Mei 17, 2018 alipofanya ziara katika eneo la Mbagala Kiburugwa na kuona badhi ya nyumba za wananchi ambazo zimeathirka kutokana na kujengwa katika maeneo hatarishi na kuwataka wakazi hao kahama mara moja.

“Nitoe rai kwa wasichana ambao hawajaolewa, usikubali kuolewa na mwanaume ambaye atakuonesha ana kiwanja bondeni, kataa huyo sio wa kukuoa sasahivi angalieni akina mama mnavyotaabika na nyumba zimebomoka hujui watoto wako unawalaza wapi” amesema Makonda.

Makonda ameongeza kuwa serikali haitaweza kutoa msaada wa chakula na malazi kila mara kwa wananchi ambao wanakumbwa na majanga yanayotokana na wao kuamua kukaa katika maeneo hatarishi kwa kujitakia.

Mkuu wa mkoa huyo amedai kuwa katika maeneo hayo ni ngumu kwa mwananchi kupata msaada wa dharura ikiwemo gari la wagonjwa au huduma ya zima moto
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad