AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Kwa mujibu wa taarifa iliyotumwa jana kwa vyombo vya habari na Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa Chadema, Tumaini Makene, kamati hiyo inakutana kujadili masuala mbalimbali muhimu kuhusu chama hicho na taifa.
Katika taarifa hiyo, Makene alisema miongoni mwa mambo makuu yatakayojadiliwa katika kikao hicho leo ni kupokea taarifa na kujadili juu ya uchaguzi wa marudio wa ubunge, udiwani na hali ya siasa nchini.
"Kikao kitafanyika jijini Dar es Salaam chini ya Mwenyekiti wa chama, Freeman Mbowe, kitajikita katika masuala mawili, kupokea taarifa na kujadili kwa kina juu ya uchaguzi wa marudio wa ubunge na udiwani na hali ya siasa nchini," alisema Makene katika taarifa hiyo na kuongeza:
"Wanachama wa Chadema na umma wa Watanzania kwa ujumla utataarifiwa kuhusu maazimio baada ya kikao hicho."
Mbali na wabunge na madiwani kujiuzulu na kuhamia Chama Cha Mapinduzi (CCM), chama hicho kikuu cha upinzani nchini kimefanya vibaya katika uchaguzi wa Jumapili kwa kulipoteza kwa wapinzani wao hao Jimbo la Buyungu mkoani Kigoma.
Uchaguzi wa marudio umefanyika katika jimbo hilo kutokana na kufariki dunia kwa aliyekuwa mbunge wake, Kasuku Bilago (Chadema).
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK