Madiwani Wengine wa Chadema Wajiunga na CCM Leo

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Madiwani Wengine wa Chadema Wajiunga na CCM
Madiwani wawili wa Chadema mkoani Kilimanjaro  wamejivua uanachama na kujiunga na CCM.

Waliohama chama hicho leo Agosti 17 ni aliyekuwa diwani wa kata ya Romu wilayani Hai, Shilyimaufoo Kimaro na diwani wa kata ya Vumari, Wilayani Same, John Msofe.

Akizungumzia kuondoka kwa madiwani hao Katibu wa Chadema mkoa wa Kilimanajro,Basil Lema amesema ni kweli madiwani hao wameondoka kwa kile wanachodai wao ni kuunga mkono juhudi za Rais.

Lema amesema kuwa anajua madiwani hao wanahama chama hicho kutokana na baadhi yao kutishiwa uhai na usalama wa maisha yao na wengine wanaondoka kwa sababu ya madeni waliyonayo au maslahi yao binafsi.

“Madiwani wanaobaki wabaki na wale wanaoondoka waondoke lakini tunajua wanaondoka kwa sababu ya vitisho wanavyopata na wengine wanaondoka kutokana na madeni walionayo wakijifanya wanaunga mkono jitihada za Rais,”amesema.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad