AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Afande Sele ametoa kauli hiyo kupitia ukurasa wake wa kijamii usiku wa leo Septemba 03, 2018, baada ya kusambaa sauti yake mitandaoni aliyokuwa akizungumzia sakata la Katibu Mkuu wa CCM, Dkt. Bashiru Ally kuwa ameona mbali kuwazuia wasanii wa bongo fleva na filamu katika shughuli za kichama. Kwa madai wapo baadhi ya wasanii hao walikuwa wakiichafua CCM kutokana na matumizi ya dawa za kulevya pamoja na picha za nusu utupu.
"Mimi ndio Mfalme wa huu muziki wa kizazi hiki, msitake kunipangia niongee hiki au hiki. Mimi naongea kile kinachostahiki chenye muelekeo wa kuitoa hii nchi kwenye dhiki na unafiki hata kama itanisababishia chuki au ikibidi kufariki, kwani hata nikikaa kimya miaka 80 sivuki", amesema Afande Sele.
Afande Sele ni miongoni mwa wasanii wakongwe wa bongo fleva ambaye alijiunga na Chama cha Mapinduzi (CCM), mnamo Machi 15, 2018 mbele ya Rais Dkt. Magufuli kwa lengo la kuunga mkono jitihada zake anazozifanya katika kupigania na kukiomba chama hicho kimpokee kama kijana wao.
Kwa upande mwingine, Afande Sele aliwahi kugombea Ubunge Jimbo la Morogoro Mjini mwaka 2015 kupitia chama cha ACT Wazalendo kabla ya kujivua uanachama na kusema kuwa hataki tena kujihusisha na siasa.
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK