Familia ya Mo Dewji yaeleza Alivyopatikana, Afya yake

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Familia ya bilionea Mohammed Dewji, imesimulia namna ambavyo kijana wao alivyoachiwa na watekaji usiku wa kuamkia leo.

Msemaji wa familia hiyo, Azziz Dewji ameviambia vyombo vya habari kuwa watekaji hao walimuachia huru bilionea huyo kijana majira ya saa 8 usiku, Oktoba 20.

Alieleza kuwa baada ya kumuachia, Mo Dewji alimpigia simu baba yake na kisha kurejea rasmi nyumbani kwao.

“Yuko hapa nyumbani tunamshukuru Mungu. Walimuachia majira ya saa nane na nusu usiku halafu yeye akapiga simu kwa baba yake,” alisema Azziz.

Aliongeza kuwa afya ya bilionea huyo ni nzuri kwa asilimia 100 na kwamba kama kuna tatizo litakuwa tatizo la kisaikolojia kutokana na kutekwa.

Aidha, alimshukuru Rais John Magufuli, vyombo vya usalama pamoja na wananchi kwa juhudi za kupatikana kwa mwanaye.

Mo alitekwa saa 11 alfajiri ya Oktoba 11 mwaka huu, katika hotel ya Colosseum iliyoko Oysterbay jijini Dar es Salaam, alipokwenda kufanya mazoezi.


Familia yake imesema kuwa itazungumza na vyombo vya habari leo kuhusu kupatikana kwa kijana wao ambapo naye atahudhuria mkutano huo.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad