Kifo cha Mtangazaji Isack Gamba..Hakufika Kazini Siku Mbili Ndipo Walipoamua Kuvunja Mlango wake

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Aliyewahi kuwa Mtangazaji wa Radio One na ITV, ambaye baadaye alijiunga na Idhaa ya kiswahili ya Radio Deutch Well ya Ujerumani(DW) Isack Gamba ameekutwa amefariki dunia mjini Bonn Ujerumani.

Taarifa za kifo cha Isack Gamba zilijulikana baada ya kutofika kituo chake cha kazi, ambapo inadaiwa kuwa amekutwa amefariki nyumbani kwake leo Alhamisi Oktoba 18, 2018.

Mmoja kati ya mfanyakazi mwenzake amesema kuwa taarifa zilizotoka nchini Ujerumani zinasema kuwa Gamba hakuonekana kazini kwa muda wa siku mbili, Jumanne na jana Jumatano Oktoba 17.

Amesema kuwa leo pia hakuonekana kazini asubuhi, ndipo watu wa ofisini wakaenda kutoa taarifa polisi, waliofika nyumbani kwake na kuvunja mlango wakamkuta Gamba amefariki tayari.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad