Usain Bolt Ppewa ofa ya mkataba wa kucheza soka

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Usain Bolt apewa ofa ya mkataba wa kucheza soka
Aliyekuwa mwanariadha maarufu wa mbio fupi duniani, Usain Bolt amepewa ofa rasmi ya mkataba wa kuichezea klabu ya Central Coast Mariners ya nchini Australia.

Bolt amekuwa akifanya majaribio na klabu hiyo tangu mwezi Agosti mwaka huu, ambapo hivi sasa amepewa ofa rasmi wa kuichezea klabu hiyo kwa mujibu wa wakala wake.

"Kujibu kuhusiana na habari zilizoandikwa, ni kweli Usain amepewa ofa ya mkataba lakini sitoweza kuongeza zaidi ya hapo", amesema wakala wa mchezaji huyo, Ricky Simms.

Usain Bolt alifanikiwa kucheza mechi yake ya kwanza ya kiushindani kwenye klabu yake mapema mwezi huu na kufanikiwa kufunga mabao mawili, jambo ambalo liliwapa matumaini klabu hiyo juu ya kumpa mkataba.

Endapo atasaini mkataba rasmi wa kuitumikia klabu hiyo, ataunganishwa katika kikosi kinachoshiriki ligi kuu nchini Australia (A-League), ligi ambayo imeanza rasmi wiki hii kwa Central Coast Mariners kutoka sare ya bao 1-1 na Brisbane Roar.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad