AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Akiwa kwenye pati hiyo, Shilole alionekana akiwa amekaa na wasanii wenzake wa kike, Mwasiti Almas na Esterlina Sanga ‘Linah’ huku akiwa na nundu usoni na mdomo wake ukiwa umechanika sehemu ya juu.
Baada ya kuona hali hiyo huku kukiwa na minong’ono kuwa huenda alipigwa na mumewe, Ashraf Uchebe, Ijumaa Wikienda lilimsogelea Shilole na kumuuliza kuliko au kuna masahibu gani yaliyomkuta ambapo alifunguka:“Aaa…Unajua juzijuzi ndiyo nimehamia nyumbani kwangu Majohe, sasa nyumba yenyewe bado sijaizoea na bado sijaweka umeme, sasa niliporudi usiku nikiwa nimechoka ndiyo nikajikuta napiga mwereka na kuumia hivi.
“Si unajua nyumba usiyoizoea? Hayo ndiyo yaliyonikuta na hii pati kwa kuwa nilishaalikwa na kumhakikishia Nandy kuwa nitakuwepo, nimeona nijikongoje nifike haina jinsi.”
Hata hivyo, licha ya kuwa na majeraha hayo, Shilole alionekana kuwa mchangamfu kama kawaida yake na kuvamia sehemu ya kuchezea kisha akatoa machejo wakati akibanjuka na kuwafanya wageni waalikwa kupiga mayowe ya kumshangilia
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK