AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Akizungumza wakati akitangaza uamuzi wa kumuweka kiongozi huyo ndani, Jerry Muro amesema diwani huyo aliyefahamika kwa jina la Dinna Erick Mbise kuwa alikabadhiwa mifuko ya saruji 41, na moja ya wawekezaji wilyani humo ambapo hakuikabidhi kwa shule husika.
Muro amesema,"Diwani huyo wa CHADEMA amechukua mifuko iliyotakiwa kwenye kujenga shule na yeye hakupeleka wiki nzima, tukisema tunaambiwa tunaowaonea wao ni CHADEMA, lakini si kitu kizuri."
"Hii ni moja ya sehemu inayofanywa na wenzetu kutukwamisha, wanazunguka kuhamasisha watu wasituchangie huku ni kutuhujumu kabisa tukiwashughulikia mnatusema hatuna demokrasia. Tunajua mmepanga kutuhujumu lakini tutawashughulikia tu", ameongeza Jerry Muro.
Mara kwa mara Mkuu huyo wa Wilaya amekuwa akiingia kwenye migogoro na baadhi ya viongozi wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA kutokana na sababu mbalimbali kutokana na kupishana mitazamo ya masuala mbalimbali nchini.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK