Iran Yasema Marekani Haiwezi Kuiangamiza

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Waziri wa mambo ya nje wa Iran Mohammed Javad Zarif amesema kile alichokiita ''kejeli za maangamizi'' za rais wa Marekani Donald Trump haziwezi kuimaliza Iran.

Kupitia mtandao wa Twitter, Zarif amesema Iran imesimama imara kwa maelfu ya miaka, wakati maadui wake wote wakiwa wametoweka.

Haya Zarif anayasema wakati mvutano ukizidi kushamiri baina ya nchi yake na Marekani, na onyo la Trump kwamba ikiwa Iran haitaacha kuitishia Marekani, basi mwisho rasmi wa Iran utakuwa umewadia.

Mahusiano baina ya nchi hizo mbili yalizidi kuzorota mwaka jana baada ya Rais Trump kuiondoa Marekani katika makubaliano kuhusu mpango wa nyuklia wa Iran, yaliyosainiwa mwaka 2015 kati ya taifa hilo la Kiislamu na nchi zenye nguvu duniani.

Mvutano huo ulichukuwa sura mpya mwezi huu pale Marekani ilipopeleka katika eneo la Ghuba manowari na ndege za kivita chapa B-52 kujibu ilichokitaja kuwa kitisho kutoka Iran ambacho haikukifafanua.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad