Juma Kaseja Alamba Mkataba wa Miaka Miwili KMC

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

KIPA Juma Kaseja ‘Tanzania One’ ameongeza mkataba wa miaka mitatu kuendelea kuitumikia klabu yake ya KMC aliyoichezea msimu uliopita.

Kaseja amesaini mkataba huo leo Jumamosi huku ukiwa ni mwendelezo wa timu hiyo kubakiza nyota wake ambao waliokuwa nao msimu uliopita.

Akiwa na kikosi hiko Kaseja amewapa changamoto makipa wenzake, Jonathan Nahimana pamoja na Dennis Richard hali iliyofanya kikosi hicho kuwa imara.

Kipa huyo ameiongoza KMC akiwa Nahodha ambapo walimaliza ligi wakishika nafasi ya nne kutokana na mwenendo mzuri ikiwa chini ya kocha Ettien Ndayiragije ambaye sasa ni kocha wa Azam FC.

Wachezaji wengine walioongezwa mikataba ni Charles Ilanfya, Dennis Richard, Rehan Kibingu, Sadala Lipangile, Cliff Buyoya, Ismail Gambo, Omary Ramadhan, Abdul Hillary, Ally Ramadhan na Rayman Mgungila.

KMC inayomilikiwa na Manispaa ya Kinondoni itashiriki michuano ya kimataifa ya Kombe la Shirikisho barani Afrika, ikiwa ni mara yao ya kwanza tangu ipande Ligi Kuu ambayo pia wamecheza msimu mmoja pekee.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad