AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Watuhumiwa hao, wanne kutoka mkoani Njombe na wanne kutoka mkoani Ruvuma wanashikiliwa na Polisi wilayani Namtumbo kwa kufanya ramli chonganishi na kutaka kumtoa kafara mtoto mdogo.
Walikamatwa katika Mlima Mgwijima wakiwa na mtoto mdogo na vifaa mbalimbali vinavyodaiwa kutumika katika kafara wakiwemo mbuzi mmoja mweusi, kuku wawili (mmoja mweusi na mwingine mweupe).
Inadaiwa Polisi baada ya kupata taarifa za kiintelijensia walifika katika mlima huo na kuwakamata watuhumiwa hao ikiwa ni pamoja na mganga wa kienyeji, lakini baada ya mahojiano walikana madai hayo.
Awali, mmoja wa watuhumiwa, mwanamke ambaye alikuwa na mtoto huyo akiwa ametokea Njombe, baada ya kufika kituo cha polisi ‘alipandisha mashetani’ na kuanza kujigaragaza akisema wale wengine hawana makosa ila yeye.
Baadaye alipotulia na kuhojiwa alikana madai hayo na kudai kuwa yeye ni mgonjwa, hivyo alioteshwa kutoka Njombe kwenda kwenye mlima huo ili kupona. Jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi wa tukio hilo.
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK