AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Dar es Salaam. Hussein Bashe amemshukuru Rais wa Tanzania, John Magufuli kwa kumteua kuwa naibu waziri wa kilimo huku akiahidi kwenda kutoa mawazo mapya ndani ya wizara hiyo inayochangia asilimia 28 ya pato la taifa (GDP).
Bashe ametoa kauli hiyo leo Jumapili Julai 21, 2019 alipokuwa akizungumza na Mwananchi saa chache kupita tangu taarifa ya Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais Ikulu ya Tanzania ilipotoka na kuelezea uteuzi huo.
“Mimi niseme tu kwanza nimshukuru Rais kwa imani yake kwangu ambayo amenipa, kwa hiyo jukumu langu nimepewa kwenda kumsaidia waziri (wa kilimo, Japhet Hasunga) kwenda kuhakikisha tunafikia malengo na matamanio ya Watanzania,” amesema Bashe ambaye ni mbunge wa Nzega Mjini
Bashe amesema, “Hii ndio sekta iliyoajili Watanzania wengi, inaendesha uchumi wa nchini inachangia 28 ya GDP na asilimia 70 ya ajira lakini ina changamoto nyingi, nina amini katika ushirikiano tutafanikiwa.”
Katika taarifa hiyo ya uteuzi, Bashe anakwenda kuchukua nafasi iliyoachwa wazi na Innocent Bashungwa ambaye aliteuliwa kuwa waziri wa viwanda na biashara.
Pia, Rais Magufuli amemtua George Simbachawene kuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira akichukua nafasi ya Januari Makamba ambaye uteuzi wake umetenguliwa.
By Ibrahim Yamola, Mwananchi
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK