AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Msanii wa Bongo fleva Rajab Kahali maarufu Harmonize ametangaza nia ya kumsaidia msanii mwenzie Aboubakary Katwila maarufu Q Chilla ili kumrudisha tena kwenye soko la muziki baada ya kupotea.
Harmonize amesema kwa kuanzia watatoa EP (albam fupi) yenye nyimbo tatu na video zake ambazo wameshirikiana kwa pamoja na wameipa jina la ‘Return of Q Chilla’ na itaachiwa Julai 22.
Akizungumza na waandishi wa habari, Harmonize amesema anamsaidia Q Chilla kwa kushirikiana na uongozi wa lebo ya WCB chini ya msanii Nasib Abdul maarufu Diamond Platnumz.
“Q Chilla ni msanii mkubwa hapa nchini na ndiyo chanzo cha maendeleo ya muziki wetu kwa kushirikina na uongozi wa Wasafi tumeona tushirikane na watanzania kuhakikisha kipaji chake hakipotei ili pia apate maisha mazuri na familia yake,” amesema Harmonize.
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK