Samatta Awakumbuka Viongozi wa TFF

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Nahodha wa timu ya taifa ya Tanzania Mbwana Samatta amebainisha kuwa amejaribu kuwatembelea gerezani viongozi wa zamani wa klabu ya Simba ambao ni makamu wa Rais Godfrey nyange 'kaburu'  na Rais wa TFF, Jamali Malinzi lakini hakufanikiwa kuwaona.

Samatta ambaye alikuwa na Taifa Stars nchini Misri ilikokuwa ikishiriki AFCON 2019 na kutolewa hatua ya makundi amesema licha ya kutowaona lakini anawaombea.

Kupitia Twitter Samatta ameandika, ''Leo nimebahatika kupita gereza la keko ili kuwaona ndugu Godfrey Nyange 'Kaburu' na ndugu Jamal Malinzi, lakini sikufanikiwa kuonana nao kutokana na sababu zilizo nje ya uwezo'', amesema.

Samatta ameongeza kuwa ''Bado naendelea kuwaombea wao na wafungwa wote, amani na furaha''.

Kikosi cha Taifa Stars kilirejea jana kutoka nchini Misri ambapo kilicheza mechi tatu za Kundi C dhidi ya Senegal, Kenya na Algeria lakini kikapoteza mechi zote.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad