AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Nyanzi amekutwa na hatia ya unyanyasaji wa kimtandao pamoja na mawasiliano ya udhalilishaji dhidi ya rais Yoweri Museveni na familia yake.
Aidha, kabla ya hukumu hiyo, Dkt. Nyanzi alikataa kumsikiliza hakimu wakati akisoma hukumu dhidi yake na badala yake kufanya vurugu kwa kuvua nguo na kuonesha sehemu ya mwili wake.
Wakati kesi ikiendelea, Dkt. Nyanzi alikataa kuomba dhamana na amekuwa katika gereza kuu la Uganda la Luzira kwa miezi minane tangu akamatwe.
Pia Dkt. amekuwa mtu maarufu sana nchini humo ambaye amekuwa akitumia lugha chafu kuukosoa hadharani utawala wa Rais Museveni kwa kuandika katika mitandao ya kijamii maneno yasiyokuwa na staha kuhusu utawala wa Rais huyo.
Dkt. Nyanzi ambaye ni mtafiti wa masuala ya jamii, kabla ya kuanza kampeni yake ya matusi kupitia kwenye mitandao ya kijamii aliwahi kuwa mhadhiri katika chuo kikuu cha umma nchini Uganda cha Makerere.
Hata hivyo, mashtaka hayo chini ya sheria ya matumizi mabaya ya kompyuta ni jaribio la utekelezwaji wa sheria ya uhalifu wa mtandaoni inayokosolewa na wengi.
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK