AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
MWANAMUZIKI wa nchini Uganda, Ziggy Wine, ambaye alikuwa chini ya usimamizi wa ‘Lebo’ ya mwanamuziki/mwanasiasa Bobi Wine, amefariki dunia usiku wa jmapili, Agosti 4, 2019.
Ziggy ambaye jina lake halisi ni Michael Kalinda, amefariki baada ya kutekwa Julai 21, mwaka huu, na kupigwa vibaya alipokuwa njiani akielekea studio za Firebase Crew. Inaelezwa kuwa baada ya watekaji kukamilisha unyama huo, walimtupa pembezoni mwa hospitali ya Mulago iliyopo jijini Kampala ambapo alikutwa akiwa amejeruhiwa vibaya huku jicho lake la kushoto likiwa limetobolewa, vidole vyake vya mkononi vikiwa vimekatwa.
Bobi Wine, Mbunge wa Kyadondo Mashariki ambaye pia alikuwa akimsimamia Ziggy kimuziki, tayari ameshazungumzia suala hilo, kupitia ukurasa wake wa Twitter ambapo ameandika:
“Ziggy alipatikana akiwa amejeruhiwa vibaya kwa kupigwa na kuteswa, jicho lake moja la kushoto likiwa limetolewa na vidole vyake viwili vikiwa vimekatwa, na zaidi ya hapo wamemuibia kila kitu alichokuwa nacho na kisha kumtupa pembeni ya hospitali ya Mulago”.
Vyanzo vya habari nchini Uganda vimeliambia gazeti la Daily Monitor la nchini humo kuwa baada ya kutekwa na kujeruhiwa vibaya, Ziggy alilazwa katika Hospitali ya Mulago kwa zaidi ya wiki moja katika kitengo cha wagonjwa mahututi lakini hakupatiwa matibabu yoyote yanayostahili kwa makusudi, kitendo kilichofanya familia yake kulalamikia uongozi wa hospitali hiyo.
Ripoti kutoka hospitali hiyo inaeleza kuwa, Ziggy amefariki baada ya kujeruhiwa vibaya sehemu ya ubongo wake, na kuwa uchunguzi wa CT Scan ulibaini kuwa kuna damu nyingi ilivujia ndani ya ubongo.
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK