Ushirika wa Bobi Wine, Besigye kutikisa kiberiti cha Museveni

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Umaarufu wa muda mfupi wa msanii, Robert Kyagulanyi “Bobi Wine” katika siasa za Uganda umeonekana dhahiri kuitia hofu Serikali ya Rais Yoweri Museveni (75) ambaye ametawala kwa miongo mitatu sasa.

Bobi Wine ambaye ni mbunge wa Kyadondo Mashariki amekuwa akikamatwa mara akwa mara na polisi na kufunguliwa mashtaka mbalimbali likiwamo la uhaini ambalo alifunguliwa Agosti 2018 kwa madai kwamba alishambulia msafara wa Rais Museveni katika mji wa Arua uliopo Kaskazini Magharibi mwa Uganda.

Rekodi yake hiyo haina tofauti sana na ya mwenzake, Dk Kiiza Besigye, mpinzani wa siku nyingi wa Rais Museveni. Sasa wawili hao wamekaa chini ya mwavuli mmoja, People’s Power, nia yao ikiwa ni kumwangusha Museveni. Swali ni je, watafua dafu au wataishia tu kutikisa kiberiti?

Ushirikiano na Besigye

Bobi Wine na Dk Besigye wameahidi kushirikiana katika kundi linaloitwa People’ Power ili kuiondoa madarakani NRM ya Rais Museveni.

Taarifa ya pamoja iliyotolewa hivi karibuni na wanasiasa hao ilieleza kuwa wamekubaliana katika kushirikiana kisiasa dhidi ya Rais Museveni.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad